Shirika la umeme Tanzania, limesema mgao wa umeme kwa sasa hauzuiliki kutokana na mabwawa yanayotumika kuzalisha umeme kukumbwa na ukame. Mkurugenzi mkuu wa shirka hilo Mhandisi Felchesmi Mramba amesema hayo kwa waandishi wa habari kuwa uzalishaji umeshuka hadi kufikia megawati 105 kutoka 561. Hivyo TANESCO kutegemea zaidi mitambo ya mafuta na gesi asilia ili kupunguza makali ya mgao huo kwa kuwasha mtambo mmoja baada ya mwingine hadi mwishoni mwa Oktoba.

Post a Comment

 
Top